• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe ya ofisi |
Tanganyika District Council
Tanganyika District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanganyika District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasissi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu, ufuatiliaji na Uchumi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Elimu Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Afya
      • Ujenzi
    • Kitengo
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
      • TEHAMA na Mahusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Miradi ya Elimu
    • Usafirishaji
    • Ufugaji Nyuki
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Leseni za Biashara
    • Uvuvi
    • Ufugaji Nyuki
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo
    • Matumizi Bora ya Ardhi
    • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Kitaifa
    • Video za Shughuli za Halmashauri
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Gazeti la Mpanda Leo
    • Makala Mbalimbali

Bandari Karema Kazini rasmi.

Posted on: September 1st, 2022

Wananchi na Wafanya biashara wasafirishaji wa bidhaa katika Mwambao wa ziwa Tanganyika wametakiwa kuachana na Bandari zisizo rasmi na badala yake kutumia Fursa ya Bandari ya kisasa ya Karema iliyoanza kutumika 1 Septemba 2022 kwa shughuli za kusafiri na Usafirishaji wa Bidhaa zao.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe.Onesmo Buswelu amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko ambapo 1 Septemba 2022 amefika katika Bandari ya Karema kushuhudia kuanza kwa shughuli za usafirishaji  Bandarini hapo.

Akizungumza  na Baadhi ya Wananchi Bandarini hapo DC Buswelu amewataka Wananchi na Wafanyabiashara wanaofanya shughuli za Usafirishaji katika mwambao wa Ziwa Tanganyika pamoja na Wananchi watakaosafiri kupitia Bandari mpya kutunza Miundombinu ya Bandari hiyo kusudi iweze kutoa huduma kwa muda mrefu zaidi.

Mhe.Buswelu ameitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania TPA pamoja na Shirika la Uwakala wa Meli Nchini TASAC kushawishi Meli  kubwa kutoka Kongo na Maeneo mengine kutia nanga katika Bandari ya Karema.

Shabani Juma, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganganyika amemshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa Bandari hiyo ambapo ametoa rai kwa Wafanyabiashara wanaosafiri kwenda Kongo kutoka Dar es slaam na Maeneo mengine Nchini kutumia Barabara ya Tabora Mpanda iliyo katika kiwango cha Lami kurahisisha kufika kwa urahisi katika Badari ya Karema.

Naye Diwani wa Kata ya Karema Bw. Michael Kapata pamoja na shukrani alizozitoa  kwa Serikali amesisitiza juu ya umuhimu wa Ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha Lami kutoka Mpanda Karema ili kurahisisha shughuli za Uchukuzi na Usafirishaji wa Bidhaa kutoka Mpanda Mjini hadi Karema Bandarini.

Kaimu Meneja Mfawidhi wa bandari za TPA Ziwa Tanganyika Edward Mabula ameeleza kuwa Zaidi ya boti 4 za Abiria pamoja na Boti za Utalii zimewasili Bandarini hapo ambapo abiria 35 wamepokelewa katika Bandari hiyo wakitokea maeneo mbalimbali ya mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Bandari hiyo iliyogharimu Bilioni 47.9 ilihusisha ujenzi wa kivunja mawimbi, mlango bandari na gati ya meta 150 zenye uwezo wa kulaza meli zenye urefu wa meta 75 na upana wa meta 15, uchimbaji na uwekaji wa kina wa mlango wa bandari, jengo la ofisi, sebule ya abiria na shehena ya jumla.

Matangazo

  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA May 27, 2025
  • WALIOITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA DEREVA II, KATIBU MAHSUSI III NA WATENDAJI WA KIJIJI III July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TANGANYIKA July 16, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • COMRADE KAWAIDA: MHE RAIS AMENIAGIZA NIFIKE KASEKESE, KUTEMBELEA MRADI WA BARABARA & KUZUNGUMZA NA VIJANA.

    June 13, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • UKUSANYAJI WA KODI WAPAA TANGANYIKA – DC: 'NDIYO NJIA PEKEE YA KULETA MAENDELEO'

    May 27, 2025
  • HALMASHAURI ZA WILAYA YA MOMBA NA MAKETE ZAKUTANA WILAYANI TANGANYIKA KUJIFUNZA BIASHARA YA KABONI.

    May 26, 2025
  • Tazama zote

video

MILIONI 328 KUKAMILISHA UJENZI WA OFISI ZA TFS TANGANYIKA, DC BUSWELU ASISITIZA UBORA WA MAJENGO.
Video nyingine

Mawasiliano ya Haraka

  • Taarifa kwa Umma
  • Orodha ya Madiwani
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA HALMASHAURI YA TANGANYIKA
  • Gazeti la Mpanda Leo
  • Habari Mpya
  • Mwanzo
  • Matukio
  • Matangazo

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikuli
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi Tanzania
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti kuu ya Serikali

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free visitor counters

Dira ya Ramani

Wasiliana Nasi

    TONGWE - MAJALILA

    Sanduku la barua: S.L.P 01 KATAVI - TANGANYIKA

    Telephone: +255-252955264

    Simu ya mkononi: 0754870344

    Barua pepe: ded@tanganyikadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sitemap
    • Huduma
    • Test

Copyright ©2018 Tanganyika-DC . All rights reserved.